Waziri wa Maji, Mh. Jumaa Aweso akishirikiana na viongozi wa Bodi ya Bonde la Wami/Ruvu kusafisha mto ili kuruhusu maji kupita kwa urahisi ili kuingia kwenye mto Ruvu na kupunguza mgao wa maji kwa wakazi wa Pwani na Dar es Salaam.
Afisa Maji Msaidizi kidakio cha Pwani, Halima Faraji akitazama jinsi maji yalivyopungua katika Mto Ruvu kutokana na kukauka kwa maji.
Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu imekabidhi Ofisi ya Jumuiya ya Watumia Maji katika Bonde dogo la Tami/Msowero wilayani Kilosa Mkoa wa Morogoro.
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mh. Selemani Jafo ametembelea Banda la Maonesho la Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu kwenye Wiki ya Mazingira Duniani.
Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Emanuel Kalobelo akijaribu kuendesha moja ya Pikipiki kati ya 18 zilizotolewa na Ofisi ya Bonde la Wami/Ruvu kupitia mradi wa uendelezaji sekta ya maji awamu ya pili kwa viongozi wa Jumuiya za Watumiaji Maji ili kuboresha usimamizi na ufatiliaji katika vyanzo hivyo.
Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu ina jukumu la kulinda, kutunza na kuhifadhi Rasilimali za maji na Mazingira kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji Namba 11 ya Mwaka 2009. Katika kutekeleza sheria hii ya kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji.